Kujenga nguvu ya pamoja katika kutetea, kulinda na kusimamia haki ma maslahi ya chama.
Kuwa chama imara, chenye nguvu, cha kidemokrasia, kinachojitegemea, kinachounganisha wafanyakazi wote kutoka sekta za ulinzi zinazowakilishwa ndani ya TUPSE, kinachotimiza haki na matazamio ya wanachama wake kwa kukidhi mahitaji yao ya kijamii.
Kuwa chama kinachotimiza haki na matazamio ya wanachama wake kwa kukidhi mahitaji yao ya kiuchumi na kijamii.
Miaka ya Uzoefu
Idadi ya wanachama
Kulinda na kutetea haki na maslahi ya Wanachama.
Kuboresha na kuendeleza hali nzuri ya Wanachama katika maisha yao wakiwa kazini.
Kujadiliana na Mwajiri kwa lengo la kuondoa tofauti zinazojitokeza baina ya Waajiri na Waajiriwa na kati ya Mwajiriwa mmoja na mwenzake.
Kutoa elimu juu ya masuala mbali mbali ya kikazi, ikiwa ni sambamba na kuwaelimisha wanachama juu ya haki/wajibu wao wawapo kazini, kupitia semina, matamasha, na mikutano.
katika uboreshaji masilahi ya wafanyakazi chama kitajikita katika kujadiliana na waajiri, serikali kwa lengo la kuhakikisha masilahi bora kwa wanachama yanapatikana, ili kuendana na gharama za maisha.
Kutoa msaada wa kisheria/ uwakilishi pale mwanachama anapopatwa na changamoto katika kazi yake, ikiwa ni sambamba na kuachishwa kazi pasipo sababu/taratibu kufuatwa.
Kushirikiana na Vyama vingine vya wafanyakazi nchini na kuhakikisha kuwa kwa ushirikiano huo haki za wafanyakazi zinalindwa kutetewa kwa pamoja. Na Kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha na kuimarisha ulinzi wa watu na mali zao.
Kwa kutambua kwamba Wafanyakazi Sekta ya Ulinzi Binafsi Tanzania katika utendaji wa shughuli zao wamekuwa wakisimamiwa na mamlaka mbili ambazo ni; Wizara ya Mambo ya Ndani ambayo kwa kiasi kikubwa inasimamia mifumo ya kiutendaji pamoja na vifaa vya kazi kama vile Siraha za Moto n.k. katika Makampuni haya; na Ofisi ya waziri mkuu(Kazi,Vijana,wazee, ajira, watu wenye ulemavu) ambayo kwa kiasi kikubwa imejikita katika kusimamia Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo mbali mbali kuhusiiana na masuala ya kiajira.
Kuwa chama bora kwa wafanyakazi wetu
Shabaha kuu ya chama ni kushirikisha wanachama katika maamuzi, kushinikiza kuwepo kwa sera za kuongeza na kupanua wigo wa nafasi za ajira, kuboresha mazingira ya kazi na kuhakikisha kuwa wanachama wanamudu maisha yao wakiwa ndani ya ajira na wakistaafu.
Bonyeza kitufe hiki kuweza kupakua fomu ya kujiunga ambapo ada ya uanachama ni 2% ya mshahara halisi wa mfanyakazi. Ada hii utaichangangia kila mwezi
Tupo JENGO LA MACHINGA COMPLEX Ghorofa ya 3, chumba namba 32
S.L.P. 25175 Dar es salaam Office Makao Makuu
Tel. +255 743 183 708 kanda ya Dar es salaam
Tel. 0 736 202 481 +255 736 202 481 0743 183 708 0653073341